Video: Uvutaji shisha kumponza Sergio Aguero mbele ya Pep Guardiola
Mshambuliaji wa Manchester City , Sergio Aguero huwenda akaingia matatani dhidi ya meneja wake, Pep Guardiola baada ya kusambaa kipande cha video kinacho muonyesha akivuta shisha akiwa sambamba na mrembo Lola Magnin.
Lo que no llegamos a mostrar en @losangeles_ok LOLA MANGIN, la nueva novia del KUN. Ya se muestran en las redes #LAM pic.twitter.com/BU9w9mzAFM
— A N G E L (@AngeldebritoOk) August 22, 2018
Mwanamitindo, Lola Magnin mwenye umri wa miaka 18, hapo jana siku ya Jumapili ameposti kipande cha video kwenye mtandao wake wa Instagram inayomuonyesha akivuta shisha yeye na nyota huyo wa Argentina huku wakiwa wenye furaha.
Video hiyo imemuonyesha Aguero mwenye umri wa miaka 30 akivuta waziwazi shisha mbele ya kamera akiwa na mrembo huyo.
Aguero aliwahi kuhusisha kutoka kimapenzi na mrembo huyo lakini alikanusha tuhuma hizo akidai kuwa hatoki kimapenzi na mtu yoyote licha ya kukiri kumfahamu.
”Sitoki na mtu yoyote, namfahamu lakini haimaanishi kuwa ndiyo natoka nae kimapenzi,” Aguero aliwahi kusikika akisema hivyo siku za nyuma kabla ya tukio hilo.