Video ya Ferooz yafunga mtaa Temeke
Jana mwanamuziki Feroozi Mrisho alikuwa akikamilisha video ya wimbo wake mpya ya Mnanda aliomshirikisha mwanadada kutoka THT, Shaz B. Video hiyo imefanyika chini ya mkono wa Adamu Juma wa Visual rab, maeneo ya Temeke.
Video hiyo iliweza kukusanya watu wengi na kufanya Adam kuwa na kazi ya ziada kupenya kwapani kwa watu ili kuweza kupata picha mzuri na Clear.
Hapa njia ilifungwa kabisa, Adam akiwa amesimama akijiuliza jinsi ya kuchukua picha za hapo.
Hapa ilikuwa zamu ya mmoja mmoja au kundi kwa kundi…
He!! Ngongoti nao walikuwepo? Na wao walionyesha mambo yao ya kucheza juu juu mchezo ambao kwa sasa unapotea pole pole kama ulivyopotea mchezo wa ‘ Super Power Ngeta Kibongee…’ na mchezo wa Mazingaombwe mashuleni..
Muogo mchungu naye alikuwepo kwenye burudani hiyo, hapa alikuwa akiserebuka na Bi Mkubwa..
Babuuuu!! akiwa na Emmy wakijitoa kimasomaso
Kweli hii ilikuwa kali… Masawe aka Temba yeye alikuwa upande wa Ngoma pamoja na mtoto wa mama Saidi aka Chege Chigunda, katika Muhogo mchungu akijiuliza aanza kucheza ngoma ya nani.