Burudani
Video ya Ommy Dimpoz ‘Wanjera’ yakamata namba 1 kwenye Top 10 ya SoundCity TV ya Nigeria
Muziki wa Bongo unazidi kupenya na kufanya vizuri katika vituo mbalimbali barani Afrika.
Video ya Omary Nyembo a.k.a Ommy Dimpoz anayewania tuzo tuzo ya Afrimma mwaka huu katika kipengele cha ‘Best New Comer’, imeongezeka kwenye orodha ya video za wasanii wa Tanzania zilizoingia kwenye chart za vituo hivyo.
‘Wanjera’ imeshika nafasi ya 1 kwenye Top Ten East ya SoundCity TV ya Nigeria wiki iliyomalizika.
Wasanii wengine wa Tanzania ambao wamewahi kufanya vizuri kwenye chart hiyo ni pamoja na Diamond, Vanessa Mdee, AY, Jux, Navy Kenzo na Yamoto Band na wengine.