Michezo
Video: Yanga yabanwa mbavu Songea
Mchezo wa duru ya tatu ya Ligi Kuu ya Vodaco baina ya mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu Tanzania Bara klabu ya Young Africans dhidi ya Majimaji FC umemalizika katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea kwa sare ya bao 1-1.
Katika mchezo huo uliyokuwa nakasi pande zote mbili timu ya Majimaji ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa mchezaji Peter Mapunda dakika ya 54 huku mchezaji wa Yanga, Donald Ngoma akiisawazishia timu yake dakika ya 79 ya mchezo.
Hili ndilo bao la Peter Mapunda akimtungua kipa wa Yanga Youthe Rostand kwa guu la kushoto.
https://www.facebook.com/azamtvtz/videos/911621709004071/
Tazama bao la Yanga lilivyopatikana kupitia kwa Donald Ngoma
https://www.facebook.com/azamtvtz/videos/911638262335749/