Videos

Video za hip hop za mtoto wa miaka 9 ‘Lil Poopy’ zazua mjadala Marekani, polisi yapanga kumkamata baba yake

Mtoto mwenye umri wa miaka 9, Luie Rivera Jr., ambaye jina lake la kisanii ni “Lil Poopy,” ameonekana kwenye video anazozipost online hususan kwenye mtandao wa YouTube, akicheza muziki na wasichana wakubwa kwa umri wake, akiendesha magari ya kifahari kama Ferrari na akirap maneno kama “coke is not a bad word.”

lil poopy

Katika video nyingine mtoto huyo anaonekana akicheza na msichana katika pozi chafu huku watu wakimtupia hela.

poopyladies

Idara ya polisi ya Brockton, Massachusetts, imewasiliana na ofisi inayoshughulikia masuala ya watoto na familia nchini humo baada ya kupokea simu nyingi kutoka kwa watu walioguswa kufuatia kuona video zake.

lil-poopy-584x350

Baba wa rapper huyo Luie Rivera ameajiri mwanasheria kujilinda na uwezakano wa kukamatwa kwa kosa la jinai.

Tazama video hii ya remix ya wimbo wa French Montana.

http://www.youtube.com/watch?v=4Hi2cTlz4Gs

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents