Picha
Viongozi wa dunia wahudhuria mazishi ya waziri mkuu wa zamani wa Israel, Shimon Peres
Viongozi wa dunia wamehudhuria mazishi ya waziri mkuu na rais zamani wa Israel, Shimon Peres.
Mazishi hayo yamegubikwa na ulinzi mkali.
Orodha kubwa ya viongozi wa mataifa mengine uliwasili kwaajili ya kutoa heshima zao za mwisho.
Wapo Rais wa Marekani, Barack Obama, Rais wa Palestina, Mahmoud Abbas, Waziri wa mambo ya nje wa Misri, Sameh Shoukry na viongozi wa Ufaransa na Ujerumani.
Rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton alikuwepo kutoa heshima zake kwa Peres