Mapenzi

Vita ya kuwania kiatu cha dhahabu Premier League

Vita ya kuwania kiatu cha dhahabu Premier League

Wakati bingwa wa Premier League akiwa tayari ameshajulikana, vita pekee kwenye ligi hiyo pendwa ulimwenguni imehamia kunako kiatu cha dhahabau ‘Golden Boot’.

1. Jamie Vardy – magoli 19 

Mshambuliaji wa klabu ya Leicester City, Jamie Vard anaongoza kwenye mbio za kuwania kiatu cha dhahabu kwa kufanikiwa kufunga jumla ya magoli 9 mpaka sasa kunako Premier League.

Kama atafanikiwa kuongoza mpaka mwishoni mwa ligi nyota huyo wa Foxes’ mwenye umri wa miaka 33 atakuwa amejinyakulia kiatu hicho cha Golden Boot kwa mara ya kwanza kunako Premier League.

Leicester striker Jamie Vardy has been leading the way in this year's Golden Boot for some time

2. Danny Ings – magoli 18 

Nyota huyo wa zamani wa Mabingwa wapya wa Premier League Liverpool anaufurahia vema msimu wake Southampton kwa kufanikiwa kufunga jumla ya mabao 18 na hivyo kushika nafasi ya pilikwenye mbio za kinyang’anyiro hicho cha ufungaji bora.

Southampton's Danny Ings moved to within one goal of Vardy courtesy of brace on Sunday

3. Mohamed Salah – magoli 17 

Mshambuliaji wa Liverpool ambaye alifanikiwa kumaliza msimu wa ligi wa 2017-18 kwa kufunga magoli 32 na kuungana na Aubameyang pamoja na Mane, Mohammed Salah sasa anashika nafasi ya tatu kwenye mbio hizo akiwa na magoli 17.

Liverpool's Egyptian forward Mohamed Salah won his second Golden Boot last season

3. Pierre-Emerick Aubameyang – magoli 17 

Kwenye nafasi hiyo ya tatu yupo pia nyota wa klabu ya Arsenal , Aubameyang ambaye mpaka sasa na yeye ameshafumania nyavu mara 17.

Pierre-Emerick Aubameyang of Arsenal also finished the 2018-19 season with 22 goals

5. Sergio Aguero – magoli 16 

Nyota wa Manchester City, Sergio Aguero anaingia kwenye mbio hizo akiwa na magoli yake 16, mabao hayo ameyafunga kwenye michezo yake 24 aliyocheza.

Manchester City forward Sergio Aguero has scored 16 goals this season but is now out injured

6. Sadio Mane – magoli 15 

Kama kawaida Liverpool imefanikiwa kumuingiza tena Sadio Mane kwenye mbio hizo za kiatu cha dhahabu kwa kufanikiwa kufunga magoli 15 mpaka sasa.

Sadio Mane, also of Liverpool, also scored 22 times as last season's accolade was shared

6. Raul Jimenez – magoli 15

Klabu ya Wolves imefanikiwa kumuingiza mchezaji wao raia wa Mexico, Raul Jimenez katika kinyang’anyiro hicho baada ya kutupia jumla ya magoli 15 mpaka sasa.

Wolves striker Raul Jimenez has notched 15 goals as his side mounts a top-four challenge

8. Marcus Rashford – magoli 14

Licha ya kusumbulkiwa na majeraha nyota wa Manchester United, Marcus Rashford amefanikiwa kufunga jumla ya magoli 14 na hivyo kuingia kwenye mbio hizo.

Manchester United forward Marcus Rashford has scored 14 goals during the 2019-20 season

8. Anthony Martial – magoli 14 

Mshambuliaji wa Man United, Mfaransa Anthony Martila ameungana na mchezaji mwenzake Rashford katika kinyang’anyiro hicho cha kuwania kiatu cha dhahabu kwa kufunga jumla ya magoli 14.

Imeandikwa na Hamza Fumo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents