Habari
Vivazi vya Barron Trump vyazua kasheshe
Vivazi vya mtoto wa Donald Trump, Barron Trump amejkuita akishambuliwa katika mtandao wa Twitter kutokana na vivazi vyake amabvyo vinapingwa kuwa havifanani na hadhi ya baba yake na mama yake.
Hata hivyo Barron amejikuta akitetewa na Chelsea Clinton, mtoto wa Rais wa zamani wa Marekani katika mtandao huo kwa mavazi yake.
Gazeti la The Daily Caller, lililipoti siku ya jumatatu kuwa mavazi ya kijana huyo wa miaka 11, yamekuwa hayaendani na heshima ya Ikulu ya nchi hiyo. Baada ya kupokea mashambulizi hayo na kutetewa mama wa kijana huyo Melina Trump alimshukuru binti wa Clinton. Awali Clinton aliwahi kumtetea Barron aliposhutumiwa na kukosolewa na hata kufanyiwa utani.
Na Laila Sued