Habari

Waandishi Arusha wagomea mkutano kudai uhuru wa mwandishi wa ITV

Waandishi wa habari wa mkoa wa Arusha kwa umoja wao wamegoma kwenda ziara ya Waziri wa Ardhi William Lukuvi na badala yake wameelekea kituo cha polisi USA River kuhakikisha mwandishi mwenzao wa ITV Halfan Liundi anaachiwa huru.

Katika hilo, azimio lililopitishwa ni kuwa wote kwa umoja wao watamtenga mwandishi yoyote atakayehudhuria na kuandika kilichojiri kwenye mkutano huo wa Lukuvi. Lihundi aliwekwa ndani na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti akimtuhumu kuripoti taarifa ya maji ambayo hakuipenda na kuwa ilikuwa ni habari ya uchochezi.

BY: EMMY MWAIPOPO

CHANZO: MTANZANIA

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents