Burudani

Wabongo wampongeza Zari kwa maamuzi yake ya kuachana na Diamond

Baada ya Zari kutangaza rasmi kuwa kwa sasa hayupo tena kwenye mahusiano na mzazi mwenzie, Diamond Platnumz imeonekana hatua hiyo kupokelewa kwa mtazamo chanya na baadhi ya mashabiki wa Diamond Platnumz hususani wanawake.

Picha inayohusiana
Diamond Platnumz na Zari

Watu wengi ambao walikuwa wanawafuatilia wawili hao wameonekana wakitoa maoni ya kumpongeza kwa maamuzi aliyoyachukua ya kumuacha Diamond Platnumz.

Baadhi ya maoni ambayo yametolewa kwenye posti ya Zari kwenye mtandao wa Instagram, yamempongeza Zari kwa kumwambia kuwa yeye ni mwanamke jasiri na anayejitambua.

Hata hivyo sio mashabiki wote wamempongeza Zari wapo baadhi yao wamemkosoa kwa maamuzi hayo kwa kumwambia kuwa amekurupuka na amefanya maamuzi kwa hasira.

Soma zaidi – Mahusiano ya Diamond na Zari bye bye

Jana Februari 14, 2018 usiku Zari kupitia ukurasa wake wa Instagram alitangaza kuwa hayupo tena kwenye mahusiano na msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ambaye amezaa naye watoto wawili.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents