Habari

Wabongo wanaohit nje: Malakai(Australia) Little Kaka (Denmark)

Wafahamu wasanii hawa wawili wa Tanzania wanaofanya vizuri nchi za nje, Little Kaka na Malakai.

Little Kaka

580471_435878826428398_2032034984_n

Rajabu Willer
ni msanii maarufu nchini Denmark. Alizaliwa February 19 mwaka 1991. Mama yake ni mtanzania. Anajulikana zaidi nchini Denmark kwa jina la Little Kaka, BIGG Kaka ama KAKA. Anafanya zaidi muziki wa dancehall pamoja na rap. Ni msanii mkubwa sana nchini Denmark.

Tazama hit yake hii ya hivi karibuni, Ingen Knive Når Vi Fester.

Malakai

406513_362874343792746_747679732_n

Malakai alizaliwa na kukulia Arusha. Miaka mingi pia aliishi Maputo, Msumbiji. Mwaka 1995 alirejea tena Tanzania. 2003 alikutana na Eliezer ‘Kidd’ Kinabo. Akiwa na miaka 14, walirekodi wimbo wao wa kwanza ‘Recess’ chini ya kundi walilolipa jina ‘M-Camp Productions. Baadaye kundi lao lilikuja kuundwa na Malakai, Kidd, K-los, Reflex na Lio.

Mwaka 2007, Malakai alienda kusoma Melbourne, Australia kuchukua masomo ya biashara. Muda mfupi baada ya kukaa huko alichukuliwa kuwa chini ya HardHustleRecordings. Bado ni member wa M-Camp Productions na H-H-R na bado ameendelea kuwa msanii wa kurekodi na producer Hip-Hop na R&B.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents