Michezo
Wachezaji 50 aghali barani Ulaya Eden Hazard amzidi mshindi wa Ballon d’Or, Cristiano Ronaldo
Shirika la tathmini za thamani za wachezaji CIES kwa upande wa soka limetoa orodha mpya ya thamani za wachezaji katika ligi tano kubwa Ulaya.
Orodha inaonyesha mshambuliaji wa Chelsea, Eden Hazard anathamani ya kuuzwa kwa bei kubwa zaidi ya mshindi wa Ballon d’Or, Cristiano Ronaldo msimu huu.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Ubelgiji ana thamani ya kati ya Pound Milioni 99 hadi Milioni 110.
Mchezaji huyo wa mwaka alikuwa wa pili kwa Lionel Messi, ambaye ana thamani ya pauni milioni 207, huku mshambuliaji wa Real Madrid, Ronaldo alishika nafasi ya tatu.