Michezo

Wachezaji wa Barcelona, Atletico na Real Madrid waweka rekodi ya kipekee kwenye fainali ya kombe la dunia

Wachezaji wa Barcelona, Atletico na Real Madrid waweka rekodi ya kipekee kwenye mchezo wa fainali ya kombe la dunia

Yakiwa yamebakia masaa kadhaa kuanza  kwa mchezo wa  fainali ya Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi  , tayari  klabu kubwa  tatu kutoka  Hispania   wachezaji   wao   watashinda kombe hilo kwa namna yoyote ile.

Ivan Rakitic akikabiliana na Luka Modric kwenye moja ya mchezo wa El-Clasico. (Wote ni wachezaji wa Croatia)

Klabu ya Barcelona ,  Real  Madrid na  Atletico  Madrid  ndio  klabu  zilizotoa wachezaji  wengi     kwenye   mchezo  wa fainali  kati ya   Croatia na   Ufaransa, wachezaji  watatu kwa kila timu.

Wachezaji wa Barcelona watakaotumikia leo timu zao za taifa ni Samuel Umtiti , Ousmane Dembele  wote Ufaransa na  Ivan Rakitic wa Croatia.

Image result for Dembele and umtiti
Samuel Umtiti , Ousmane Dembele

Wachezaji kutoka Real Madrid ni Luka Modric na   Mateo Kovačić   wote wa Croatia   huku Raphael Varane  akiitumikia Ufaransa.

Image result for Luka Modric and Mateo Kovačić
Luka Modric na   Mateo Kovačić

Kwa upande wa Atletico Madrid , wachezaji watakaoiwakilisha klabu hiyo kwenye mchezo wa fainali ni   Sime Vrsaljko kutoka  Croatia na   Lucas Hernandez  na   Antoine   Griezmann   wote wa Ufaransa.

Related image
Lucas Hernandez  na   Antoine   Griezmann

Katika maana nyingine ni kwamba klabu hizo kwa matokeo yoyote yale ni lazima  wachezaji wao wachukue kombe la Dunia leo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents