Burudani

Wadukuzi wa mitandao waiingilia ‘Natamba’ ya Aslay

Kwa sasa ukimtaja Aslay basi hautaacha kutaja uwezo wake aliyonao katika muziki wa Bongo Flava, kwani amesha toa hits kadhaa kwa kipindi kifupi ikiwemo ‘Natamba’ ambayo imezua kizaazaa katika mtandao wa YouTube.

Ngoma ya ‘Natamba’ ilikuwa namba mbili trending siku ya jana  YouTube, ila kutokana na hali ya sinto fahamu ngoma hiyo imepotea katika mtandao huo na kushuka kabisa katika nafasi iliyokuwepo.

Kwa mujibu wa meneja wake MX Carter ameripoti kusikitishwa na tukio hilo na amedai kuwa kuwepo kwa  watu  wasiopenda maendeleo ya msanii huyo na kuamua kuiripoti ‘Natamba’ ishuke Youtube.

“Naona wabaya wasiopenda maendeleo ya AslayIsiaka wamereport video ishuke YouTube… bahati nzuri team ya ufundi inajitaidi kuweka sawa,” ameandika Mx katika Twitter.

Akaongeza kuandika katika mtandao wa Instagram “Poleni kwa mnaopata usumbufu kuiona Video mpya ya AslayIsihaka kama ujumbe unavyoongea hapo juu tuko kwenye jitiada za kuirudisha popote ilipokuwa ikionekana haswa kwenye trending mungu akipenda. Video imekuwa reported na iko Undereview na Youtube na tunajitaidi kuiweka sawa! Ukitaka kuangalia video ya aslay for Now ingia kwenye Bio yake au Search on YouTube.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents