Habari

Wafanyakazi wa hoteli wavuliwa nguo zote kwa shutuma za wizi Nigeria

Kundi la wakili wa haki za binadamu mjini Warri, kusini mwa Nigeria, linatafuta fidia ya kuwalipa wafanyakazi wanne ambao walidaiwa kuvuliwa nguo na mwajiri wao.

hotel

Wafanyakazi hao wanashutumiwa kuiba fedha za wageni, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti baada ya kuambiwa na baadhi ya wageni.

Wafanyakazi hao walikuwa wanne, watatu wakiwa wanawake na mmoja mwanaume waliamuriwa kuvua nguo na kuvua nguo huku polisi wakiwa wanashuhudia.

Picha na video za wahanga hao wakiwa wamesimama bila nguo zilitumwa na wengi mtandaoni.

Wakili wamemuandikia barua mmiliki wa hoteli ambaye ni Waziri wa zamani wa Nigeria kwa kuvunja sheria kwa udhalilishaji na kuingilia faragha ya wengine.

Wakili hao wanamtaka aombe radhi umma pamoja na kulipa fidia kwa wafanyakazi aliowadhalilisha.

Waliofanyiwa vitendo wanadai picha zilizorushwa mtandaoni zilikuwa zinawadhalilisha.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents