Habari

Wafanyakazi wa serikali za mitaa walia na udhalilishwaji

Chama cha wafanyakazi wa Serikali za mitaa (TALGWU)kimewatata viongozi wa kisiasa kuacha udhalilishaji kwa watendaji ngazi za kata,vijiji na mitaa.

Akizungumza na waandishi wa habari,Katibu mkuu wa chama hicho, Rashid Mtima alisema tayari wameshapeleka barua kwa makatibu tawala kwa lengo la kukusanya matukio hayo ya udhalilishaji.

“Kwa mfano tunakumbuka lile tukio la afisa ardhi aliyedhalilishwa na Makonda hivi karibuni, basi huko kwenye halmashauri, watendaji wa serikali za mitaa wananyanyasika sana,” alisema Mtima.

“Akikosea achukuliwe hatua lakini ni vyema akiachwa akajieleza, zipo taratibu za kufuata na sio kufuata umaarufu kwa njia hizo, tunaamini njia ya mazungumzo ndiyo njia sahihi tunaamini hali kama hiyo haitajitokeza tena”.

BY:Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents