Burudani

Wakazi ataja kilichomkasirisha hadi kumchana Godzilla

Rapper kutoka kundi la SSK, Wakazi ameamua kutoa yake ya moyoni kwa msanii Godzilla.

Wakazi ambaye Ijumaa hii ameachia wimbo ‘Zillnass’ aliomchana rapper huyo, amesema amekkasirishwa na kitendo cha Godzilla kummuita Nikki Mbishi kuwa ni wack wakati anasahau na yeye ni mtu feki ambaye anauiga umarekani wakati hajawahi kufika.

“Nilikashirishwa sana na Godzila kumuita Niki Mbishi wack coz ni moja ya wasanii ambao wapo kwenye top five yangu then mtu unamuita hivyo unataka watu wamchukuliaje?,” Wakazi amekiambia Bongo flava Top 20 ya East Africa Radio.

“Alichokiimba Zilla ni kile kile anachokifanya siku zote, yaani amerudia rudia maneno hana maneno mapya. Watu wanashangaa anadai ni freestlye,” ameongeza. Wakazi amesisitiza kwa kusema kuwa diss track aliyoitoa Zilla ya kawaida sana.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents