Habari
Wakazi wa Magomeni Kota wamuombea Rais Magufuli akamilishe ujenzi wa nyumba zao
Wakazi wa Magomeni kota wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, wamefanya ibada maalum kwaajili ya kumuombea Rais Dkt John Magufuli ili aweze kutekeleza azma yake kukamilisha ujenzi wa nyumba zao.
Akizungumza katika ibada hiyo, mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi, aliwapongeza wakazi hao kwa hatua hiyo na kuwaahidi ushirikiano wake, akiwa msaidizi wa Rais Magufuli wilayani humo.
“Tutapambana kuhakikisha kwamba yale aliyoyaagiza mheshimiwa rais na yale anayokusudia kuyafanya,sisi kama wasaidizi wake tunafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kwamba tunayasimamia na yanatekelezwa,” alisema.
Moambezi hayo yalijumuisha viongozi wa dini mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali.
BY: EMMY MWAIPOPO