Wakenya hawakamatiki kwenye riadha, Mwingine aweka rekodi mpya duniani (+video)
Mwanariadha kutoka nchini Kenya, Geoffrey Kamworor (26) amevunja rekodi ya dunia katika mbio ndefu za Copenhagen Half Marathon, zilizofanyika leo Jumapili Septemba 15, 2019 nchini Denmark.
Kwenye mbio hizo za kilometa 21, Kamworor alitumia muda wa dakika 57:01. Na kuweka rekodi mpya ya kutumia muda mfupi zaidi wa Half Marathon duniani.
Kamworor ambaye ni bingwa mara tatu wa mbio hizo, Amevunja rekodi ya Mkenya mwenzie, Abraham Kiptum ya kukimbia umbali huo kwa dakika 58.01, Ambayo aliiweka katika mbio za Valencia Half Marathon mwezi Oktoba mwaka jana.
Tayari shirikisho la riadha ulimwenguni (IAAF). Limeiweka rekodi hiyo mpya ambayo ilikuwa inashikiliwa na Abraham Kiptum kwa muda wa dakika 58:18.
WORLD RECORD@GKamworor smashes the half marathon world record*💥
The Kenyan ran an incredible 57:59 (unofficial and subject to ratification)🇰🇪 pic.twitter.com/cNqWgJrCuU
— World Athletics (@WorldAthletics) September 15, 2019