Michezo
”Wale wengine ni timu ya Mwabwenyenye tu, utakufa wewe kabla ya Yanga,”- Jerry Muro aunguruma (+Video)
Aliyekuwa Msemaji wa klabu ya Yanga, Jerry Muro ametangaza kurejea ndani ya timu hiyo licha ya kudai kuwa sio kwenye nafasi kama ile aliyokuwa nayo hapo awali bali ni katika kutoa mchango wake katika kipindi hiki ambacho Wananchi hao wanaonekana kama wana hujumiwa.