Michezo

Wales yatinga nusu fainali ya Euro 2016, ni vita kati Ronaldo na Bale

Hatimaye timu ya taifa ya Wales imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali baada ya kuifunga Ubelgiji kwenye michuano ya Uero inayoendelea huko nchini Ufaransa.

35DF3C0700000578-3670048-image-m-106_1467411341405

Wales wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa jumla ya magoli 3-1 huku magoli yao yakifungwa na Williams kwenye dakika ya 30, Robson-Kanu dakika ya 55 na Vokes 85 huku goli la kufutia machozi la Ubelgiji likifungwa na Nainggolan kwenye dakika ya 13.

35DF35CB00000578-3670048-image-a-97_1467409182267

Hivyo basi timu hiyo ya Wales itakutana na timu ya taifa ya Ureno kwenye mchezo wa hatua ya nusu fainali huku fainali ya michuano hiyo ikitarajiwa kuchezwa Julai 10 mwaka huu.

35DD8C4400000578-3670048-image-a-23_1467401165959

Aidha michuano hiyo inaendelea leo kwa kuzikutanisha timu ya mabigwa wa dunia, Ujerumani itakayocheza na Italia.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents