Habari

Waliopanga maandamano ya jana UDSM kukiona

Wanafunzi walioandaa mgomo wa jana Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) huenda wakakumbwa na hatua za kinidhamu kwa kosa la kukikuka sheria ndogo ya Chuo kwa kuandaa mkusanyiko pasipo kibali cha uongozi.

dsm

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo taaluma Florens Luoga amesema kuwa hadi sasa mamlaka za nidhamu chuoni hapo zinendelea na uchunguzi kubaini nani alihusika na ni kwa namna gani na baada ya hapo hatua za kinidhmu zitafuata.

“Taratibu na sheria ndogo za chuo haziruhusua mtu kuandaa mkusanyiko ambao haujaidhinishwa na menejimenti na kimsingi taratibu hizo lazima ziheshimiwe ili kuzifanya kuendelea kuwa imara hivyo tunasubiri ripoti ya walio husika endapo itaonesha kuwa wanamakosa basi watachukuliwa hatua za kinidhamu,” amesema Luoga.

Source: Mwananchi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents