Michezo

Wanachama puuzeni propaganda tupo vizuri  – Yanga SC

Uongozi wa Young Africans Sports Club umewashukuru wanachama,wapenzi na mashabiki wote kwa kujitokeza kwa wingi kuisapoti timu yao pendwa kwenye mchezo wa ligi kuu siku ya jana, pia unawashukuru wale wote ambao hawakupata nafasi ya kufika uwanjani lakini kwa namna moja  ama nyingine walikuwa sambamba na timu.

Klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya Jangwani umewaomba wanachama na wapenzi wote kupuuza propaganda zote zinazoenezwa na wasioitakia mema klabu hiyo na kusisitiza kuwa wana kikosi kizuri ambacho kina uwezo mkubwa wa kushindana na kutetea ubingwa wao na jambo muhimu ni kuendelea kujitokeza kwa wingi viwanjani na kutoa ‘sapoti’ kwa wachezaji wao huu nimwanzo wa ligi lakini wamejipanga vyema kuhakikisha wanakuwa mabingwa kwa mara ya nne mfululizo.

Yanga imesema kuwa wachezaji wao majeruhi (Chirwa, Mwashiuya,Tambwe,Benno) halizao zinaendelea kuimarika na upo uhakika mkubwa kuwa watakuwepo kwenye michezo ijayo huku swala la mchezaji, Pius Buswita likiwa linashughulikiwa.

By Hamza Fumo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents