Wanaume TMK wampa shavu Fella
Kundi la Wanaume TMK family wako mbioni kutoa album yao wakiwa
wamemshirikisha meneja wao Mkubwa Fella na album hiyo itaenda kwa jina
la "Mkubwa na Wanawe".
Itakuwa na jumla ya nyimbo 10, katika hizo nyimbo 3 ameimba Mkubwa Fella mwenyewe na wimbo mmoja ameimba na kundi nzima.
Mkubwa
Fella amewataja baadhi ya wasanii waliopiga collabo katika albamu hiyo
kuwa ni Jay Mo, Kasim, Tunda Man, Shirko, Bwana Misosi, Bashal, Dully
Sykes na Dreeze Chief.