Michezo
Wanawake wajawazito kukosa Olimpiki Brazil
Mashindano ya Olimpiki mwaka 2016 yata fanyika Brazil katika Jiji Rio De Jeneiro mwezi Agosti Wanawake wajawazito wameshauriwa kutosafiri kwenda kushuhudia kwa sababu ya hatari ya virusi vya Zika.
Serikali ya Brazil imesema kuwa hawashauri wanawake wajawazito kwenda kwenye michezo ya Olimpiki.
Hatua hii imekuja punde baada ya shirika la afya duniani WHO kutangaza hali ya dharura kutokana na madhara yatokanayo na virusi vya Zika.