Burudani
Wanawake wanne waliomzalia watoto 7 rapper Lil Boosie waanzisha reality show yao
Wanawake wanne waliomzalia watoto rapper aliyetoka jela hivi karibuni, Lil Boosie wameanzisha reality show yao.
Vyanzo vimeuambia mtandao wa TMZ, kuwa wanawake hao wa Boosie, Walnita, Tracey, Trivia, na Gerlissa wametayarisha episode ya majaribio miezi kadhaa iliyopita wakati rapper huyo alikuwa jela. Kwa pamoja wamemzalia rapper huyo watoto saba wenye umri wa kuanzia miaka 4 hadi 11.
Show hiyo itakuwa ikiangalia urafiki usio wa kawaida wa wake wenza hao na haijulikani kama rapper huyo ambaye jina lake ni Torrence Hatch atakuwa akionekana pia.