Wanawake watakaotoa mimba kunyongwa hadi kufa
Jopo la wanasheria mjini Austin, Texas nchini Marekani limepeleka muswada wa kutaka wanawake wanaotoa mimba katika jimbo hilo kunyongwa.
Tayari muswada huo umeshawasilishwa bungeni na huenda muswada huo ukapitishwa na kuwa sheria rasmi, hii ni baada ya wabunge wengi mwezi uliopita kuunga mkono kampeni ya ‘Zaa kutunza Mazingira’.
Akikazia muswada huo, Mbunge wa Dallas kwa tiketi ya Democratic, Victoria Neave amesema muswada una lengo la kukabiliana na mauaji ya vichanga ambaqvyo havina hatia na wanawake wengi wanaonekana kutojali.
“Katika uumbaji tunaamini kuwa kichanga ni binadamu kama sisi, hivyo kutoa mimba ni uuaji na ndio maana tunataka wanawake wote watakaotoa mimba nao wanyongwe kwani ni wauaji,“ameeleza Bi, Neave.
Muswda huo utajadiliwa zaidi bungeni wiki ijayo, ingawaje bado kuna baadhi ya wabunge wa chama cha Democratic wanapinga muswada huo.
Chanzo: http://www.fox32chicago.com/news/national/texas-lawmakers-consider-the-death-penalty-for-abortion