Burudani
Warembo Mbugani
Warembo wa Miss Tanzania 2010 wapo katika ziara yao ya kutembelea vivutio vya Utalii vilivyopo Mikoa ya Kaskazini, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani.
Warembo hao walitembelea Hifadhi ya Ngorongoro kujionea wanyama na mambo mbali mbali yalipo katika hifadhi hiyo, walipata pia nafasi ya kucheza ngoma ya Kimasai wakati walipokaribishwa katika Boma la wafugaji hao.