Warembo wanusurika kifo
Washiriki watano wa Miss Tanzania 2010 walinusurika kifo jioni hii baada ya boti waliyokuwa wamepanda kupindukia baharini karibu na hoteli ya Giraffe.
Kwa bahati nzuri wote walisalimika lakini walikuwa na hali ya mshtuko huku presha zikiwapanda. Kilichoshangaza wengi ni ukosefu wa askari wa majini na huduma ya kwanza kwa washiriki hao.
Mpaka sasa hajapatikana msemaji kutok kamati ya Miss Tanzania kuweza kulizungumzia suala hili.
Picha kwa hisani ya mdau wetu Amby