Wasanii 8 wa Bongo Fleva watoka kapa tuzo za AFRIMMA 2018, Uganda na Kenya waiwakilisha vyema Afrika Mashariki
Leo alfajiri kulikuwa na sherehe za utolewaji wa tuzo za AFRIMMA 2018 Mjini Dallas, Texas Marekani ambapo tumeshuhudia kwa mara nyingine Wasanii kutoka Tanzania wakishindwa kufurukuta Licha ya kutajwa kwa wingi kwenye tuzo hizo.
Tanzania ambayo ilikuwa inawakilishwa na wasanii kama Alikiba, Nandy, Vanessa Mdee, Ommy Dimpoz, Harmonize, Navy Kenzo na Jux wote wameshindwa kuchukua tuzo hizo isipokuwa Diamond aliyechukua tuzo moja ya kolabo ya mwaka kupitia African Beauty.
Afrika Mashariki wengine waliotamba ni Khaligraph Jones kutoka Kenya ambaye ameshinda tuzo kwenye kipengele cha ‘Rap African Act’ huku Eddy Kenzo na Ykee Benda kutoka Uganda wakichukua tuzo ya ‘Best Male East Africa’ na ya Msanii chipukizi.
Wengine walioshinda ni Fally Ipupa kakwara tuzo mbili ya Msanii bora wa mwaka na ile ya Leadership In Music.
Yemi Alade, Wizkid na Mr. Flavour hao wameshinda tuzo moja moja kwenye usiku huo uliokuwa unasubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki.
Licha ya kuwa Harmonize hajashinda tuzo, lakini alikuwa ni moja ya wasanii waliotumbuiza kwenye usiku huo wa ugawaji wa tuzo.
Wengine waliokuwa wanaiwakilisha Tanzania ni DJ-D Ommy, Tudy Thomas na Moses Iyobo ambaye alikuwa anawania kipengele cha Mtumbuizaji bora wa Mwaka.
Tazama orodha kamili ya washindi wa tuzo hizo.
AFRIMMA 2018 Awards & Music Festival Full WINNERS List
Best Male West Africa
Davido – Winner
Best Female West Africa
Yemi Alade – Nigeria -Winner
Best Male East Africa
Eddy Kenzo – Uganda – Winner
Best Female East Africa
Sheebah Karungi – Uganda – Winner
Best Male Central Africa
Fally Ipupa – Congo – Winner
Best Female Central Africa
Daphne – Cameroon – Winner
Best Male Southern Africa
Nasty C – South Africa – Winner
Best Female Southern Africa
Ammara Brown – Zimbabwe – Winner
Best Male North Africa
Ihab Amir – Morroco – Winner
Best Female North Africa
Souhila Ben Lachhab – Algeria – Winne
Best African Group
Toofan – Togo – Winner
Crossing Boundaries With Music Award
MHD – Guinea/ France – Winner
Best Gospel
Papa Dennis – Kenya – Winner
Best Newcomer
Ykee Benda – Uganda – Winner
Artist of The Year
Fally Ipupa- Congo – Winner
Best Live Act
Flavour – Nigeria – Winner
Best Video Director
Godfather Productions- South Africa – Winner
Best Dj Africa
Dj Dollar – Senegal – Winner
Best African Dj USA
Dj Ecool – Nigeria – Winner
AFRIMMA Video of The Year
Wizkid – Soco – Winner
Music Producer of The Year
Masterkraft – Nigeria – Winner
Best African Dancer
Diddi Emah – Nigeria – Winner
Best Rap Act
Khaligraph Jones – Kenya – Winner
Best Collaboration
Diamond Platnumz ft Neyo – African Beauty – Winner
Song of The Year
Wizkid – Soco – Winner
Best Lusophone
Kyaku Kyadaff – Angola – Winner
Best Francophone
Toofan – Togo -Winner
Best African Dancehall/Reggea Act
Burnaboy – Nigeria – Winner
AFRIMMA ACHIEVERS AWARD
Bismack Biyombo – DRC – Winner
HONORARY CATEGORIES
AFRIMMA HUMANITARIAN AWARD
Flavour
AFRIMMA SHINING STAR AWARD
Semah
AFRIMMA BEACON OF HOPE AWARD
Queen Julie Endee
AFRIMMA EXCELLENCE AWARD
Erykah Badu
AFRIMMA LEADERSHIP IN MUSIC AWARD
Fally Ipupa