Wasanii50 wa muziki wa kizazi wamekamilisha video ya maalum ya kuadhimisha miaka 50 ya amani, kwa kuimba wimbo wa pamoja katika viwanja vya taifa katika kuadhimisha miaka 50 ya amani nchini. Akizungumza na mwandishi wa safu hii, kiongozi wa kundi la Tmk Wanaume Saidi Fella ‘Mkubwa Fella’ amesema lengo la wasanii ni kuwakumbusha Watanzania kwamba miaka 50 na chaguzi nyingi zimepita ni jambo la kujipongeza.
Wasanii 50 na wadau mbalimbali waliudhulia tamasha hilo la video na waziri wa michezo, wakiwemo wanamitindo , Miongoni mwa wasanii waliokuwemo ni Joseph Haule ‘Prof J’, Amani Temba ‘Mh Temba’, Abwene Yesaya ‘Ay’, Mwijuma Hamisi ‘Mwana Fa’, Abdull Syskes ‘Dully Syskes’, Estarina Sanga ‘Linah’ na Madee.
“Ni wimbo ambao tunashukuru kwa watanzania kudumisha amani miaka yote hiyo, pia tunakumbushana kwamba amani ni jambo la muhimu sana” alisema Mkubwa Fella.