Wasanii maarufu wa muziki nchini wanaoguswa na hali ya elimu nchini Tanzania wameachia video ya kipekee ya wimbo wa Tokomeza Zero wenye lengo la kuelimisha, kuburudisha na kuitaka jamii nzima kuipa kipaumbele sekta ya elimu.
Wimbo huo umeimbwa na Mwasiti, Linah, Roma, Stamina, Maunda Zorro, Peter Msechu, Mwana FA, Linex, Keisha, Diamond na Kala Jeremiah.