Bongo Movie
Wasanii wa filamu Tanzania kuja na ‘siku ya mastaa wa filamu’
Wasanii wa filamu nchini wanatarajia kufanya tamasha kubwa lililopewa jina la ‘Siku ya mastaa wa filamu Tanzania.Tamasha hilo litafanyika tarehe 26 January kwenye viwanja vya Dar Live jijini Dar es Salaam.
Lengo la tamasha hilo ni kuchangia ofisi za shirikisho la filamu Tanzania( TAFF) ambapo kutakuwa na burudani mbalimbali kutoka kwa bendi ya Twanga pepeta, Tunda Man, Vitalis Maembe, Shilole, Snura, Kitale, Joti, Mpoki na wengine.