Habari
Wasanii wajiunga na CHADEMA
Baada ya Nakaaya Sumari kuingia rasmi CHADEMA wasanii wenzake maarufu nchini Tanzania Joseph Mbilinyi aka Sugu, Fred Malick aka Mkoloni na Gerald Mwanjoka aka G Solo wamejiunga rasmi na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kukabidhiwa kadi zao za uanachama.
Tukio hilo limefanyikai katika Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA, zilizopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Pichani ni wanamuziki hao na Kaimu Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mnyika.