Watakaobainika kuwapa ujauzito wanafunzi kukiona chamoto
Watakaobainika kuwapa ujauzito wanafunzi kukiona chamoto
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeweka sheria kali zinazowalinda watoto wa kike na watakaobainika kuwapa ujauzito na kukatisha masomo yao adhabu watakayoipata hawatoisahau maisha.
Majaliwa ameyasema hayo hapo jana siku ya Jumapili ya Julai 29, 2018 wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Mwakizega wilaya ya Uvinza akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Kigoma.
Alisema Serikali itatoa adhabu kali kwa mtu atakayebainika kukatisha elimu ya mtoto wa kike iwe kwa kumuoa au kumpa ujauzo huku akiongeza kuwa watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii na waachwe waendelee na masomo yao kwani elimu ni haki yao ya msingi.
“Tukikukuta na mwanafunzi wa kike kwenye kona zisizoeleweka adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka 30 gerezani, hivyo vijana kuweni makini,” alisisitiza.
Pia Waziri Mkuu aliwataka wazazi na walezi kushirikiana na Serikali kuhakikisha watoto wa kike wanapelekwa shule na wanamaliza masomo yao.
Waziri Mkuu aliwaasa wanafunzi wote kusoma kwa bidii ili watimize ndoto zao na wasikubali kushawishika kwa kuwa watashindwa kufikia masomo yao.
Mamaaaaaah duuuuuh m nitakuwa mgen wa nan nixhatia mimba tatu nauyu mwingne jana kaniambia ajazona cku zake m cnitauzea jela
Auta ozea jela Bali piga hesabu za hizo mimba 4 alafu zidisha Mara 30 utapat miaka ambayo utakua gerezani ukifunzwa adabu
Nitaozea jela mm jaman atangeludixhwa nilipotoka nikazaliwa upya nafikixha mwaka nipojela hata hivyo ncngetoboa jaman nitafutien mganga au kama kunamtu babuyake mganga ama ndugu yake anixaidie ncendejela mm
ndio vzr mheshimiwa maana wanaume wamezidi kutongoza tongoza ovyoooo 30 itawahusu
Wanafunzi wakike chips zinawaponza sana badirikeni wanaume msiwalaumu peke yao
Mnapenda vitu vzr mno acheni kutaman
haaaaaaaa!!! me co mwanafunzi chipsi nakula vzr tu kwa pesa yangu
haya ndo mnavyosema
ndio