Watakaotembea Dodoma bila vitambulisho vya taifa kuhojiwa na Jeshi la Polisi
Kama una desturi ya kutembea bila kitambulisho chako cha Uraia na ni mkazi wa Jiji la Dodoma basi acha mara moja tabia hiyo kwani Jeshi la Polisi Mkoani humo limeanza mchakato wa kuwahoji watu wote watakaokamatwa hawana vitambulisho vya Uraia.
Kauli hiyo imetolewa jana Agosti 7, 2018 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge ambapo ameagiza wakazi wa Dodoma kutii agizo hilo kwani limeanza kutekelezwa huku akiwataka watu ambao vitambulisho hivyo kwenda mara moja NIDA kushughulikia mchakato wa kuvipata.
“Sasa niwaombe wananchi wa Dodoma na maeneo mengine, kwamba sisi tutafanya msako tunataka Dodoma pawe salama. Na ni vizuri Kuanzia sasa nimeongea na NIDA kwamba zoezi la kutoa vitambulisho vya uraia linaisha mwezi Desemba mwaka huu, tutataka kila atakayekuwa na kitambulisho atembee nacho, ndio utambulisho wake, tutakuhoji kwa kitambulisho chako. Na ni practice ya dunia nzima.“amesema Mahenge.
Kwa upande mwingine, RC Mahenge amesema mpango huo wa serikali mkoani Dodoma ni moja ya mikakati ya kuimarisha ulinzi na Usalama wa jiji la Dodoma kutaka kuwa jiji la mfano Tanzania.
Njooon mnihoji sina kitambulisho nipo dodoma mjini kitambulisho cha taifa sijapata nipo hapa stend kubwa
Pumbavu kabisa hivyo vitambulisho mmevitoa kwa Wanainji asilimiangapi
wengine bado atujaletewa hivyo vitambulisho
😂😂😂😂😂😂 tutanyooka tu
Huo ubaguzi Sasa
Mkuu Wa mkoa hujiuliz vitambulisho havija toka
Unaifanya Dodoma yakwako
Bas tupe vitambulisho
Kieeehhh. ….tabu sana
Hahaha
Sasa hii nchi vipi hii. Ovyoovyo tu
tunaelekea nchi ya ahadi tulieni
Mm kwetu hukohuko na nampango wa kurud Mambo yakinoga na cna hicho ktambulisho tutapambania hapo.
Mwaka wa shetani msemo wa temba
Mpuuzi mwingine huyu kwani dodoma ni nchi?
Hata kwa passport ndaludi kujumiika nany
#ngosha_mwanza_mwanza
hakuna lolote pakame nan anapataka? hakuna hata kivutio cha utaliii pa nn sas
Watapata tabu saana kipigo chake kitakuwa ni cha mbwa koko
Tena ikiwezekan JWTZ maan kuna watu manunda sana itabd wafunzwe kidogo