Habari
Watanzania naomba mniombee – Rais Magufuli
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amesema kuwa anaomba siku zote Watanzania wamuombee ili ashinde vita ya uchumi.
Rais Magufuli ameyazungumza hayo Manyara wakati akizungumza na wakazi wa Simanjiro ambapo amesema kuwa Tanzania haikuumbwa kwaajili ya mafisadi.
“Ndio maana naomba siku zote ndugu zangu Watanzania naomba mniombee naomba tusimame pamoja ili tusimame pamoja tukashinde vita hii kwa maslahi ya Watanzania hasa Watanzania masikini. Leo nimekuja hapa ninajua nimekuja kufungua barabara nitaifungua lakini ngoja tuzungumzie suala la Tanzanite kwanza,” amesema Rais Magufuli.
Katika hatua nyingine Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania haikuumbwa kwaajili wa mafisadi, Tanzania imeumbwa kwaajili ya wanyonge.”