Habari
Watanzania wafurika kuuaga mwili wa ‘Akwilina Akwilini’ jijini Dar es salaam (+Picha)
Mamia ya Watanzania wamefurika kwenye viwanja vya Chuo cha Usafirishaji (NIT) Mabibo jijini Dar es salaam kuuaga mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa chuo hicho, Akwelina Akwelini ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi Ijumaa ya wiki iliyopita kwenye maandamano ya CHADEMA.
Waziri wa Elimu, Professa Joyce Ndalichako, na Mhe Mnyika pamoja na viongozi wengine wa serikali wamehudhuria misa ya kuuaga mwili wa mwanafunzi huyo.