Bongo Movie
‘Watasubiri sana’ asema Irene Uwoya huku akionesha ‘Range Rover’ yake mpya kwenye Instagram (picha)
Ukikutana na Irene Uwoya anaendesha Range Rover nyeusi, usifikiri ameazima, ni ya kwake na kwa mujibu wa maneno yake mwenyewe, ‘haters watasubiri sana’.
Irene ameshare picha akiwa amepiga juu ya Range Rover hiyo mpya, ambayo yeye anaiita ‘My Baby’ na kuandika maneno ya ‘kuumiza roho’ kuwakata kilimi wale wanaomdhania kuwa yupo ‘cheap’.
“Acha nifurahiiii banaaa…..sio mchezo,” ameandika muigizaji huyo.
Kwenye picha nyingine aliyolala juu ya gari hilo na kuyaacha mapaja yake wazi yaliyowatoa ‘udenda’ wanaume wenye uchu, Irene aliandika ‘I don’t care..’
Bongo movie inalipa..