Habari
Watu 10 watiwa mbaroni kwa kumchapa mwanamke hadharani mkoani Mara
Kufuatia tukio lililotokea hivi lililoonyesha mwanamke mmoja akichapwa viboko visivyo na idadi mbele ya umati wa watu, Jeshi la Polisi limewatia mbaroni watu kumi kwa kuhusika na tukio hilo lilitokea mkoani Mara.
Hii taarifa ya jeshi hilo:
https://youtu.be/LbI_OnfbGVM
Hivi karibuni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangallah alisema serikali imepinga vikali kitendo hicho huku ikisisistiza kutofumbia macho matukio kama hayo.
BY: Emmy Mwaipopo