Habari

Watu 29 wajeruhiwa kwenye ajali baada ya treni kugongwa na lori mkoani Dodoma

Watu 29 wajeruhiwa kwenye ajali baada ya treni kugongwa na lori mkoani Dodoma

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi amebainisha kuwa ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo ambapo Lori liligonga treni.
Treni hiyo iliyokuwa inatoka Tabora kwenda Dar es Salaam ilipata ajali kabla ya kuingia stesheni ya Dodoma na kuanguasha mabehewa yake matatu, Kw3a mujibu wa Mwananchi digital, Ajali hiyo imetokea jana saa 5.30 usiku.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, @patrobas_katambi_ ameeleza leo asubuhi kuwa ajali hiyo imetokea saa 5.30 usiku.

Amesema ametoa maagizo kadhaa ikiwemo kumsaka dereva wa lori ambaye inasemekana aliruka kutoka kwenye lori baada ya ajali hiyo.
Tutawaletea taarifa zaidi kutoka Mamlaka husika.

By Ally Juma.

 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents