Burudani

Watu na mashabiki wao buaana! Bruno Mars aingiza $240m kwenye 24K Magic World Tour

Watu na mashabiki wao buaana! Bruno Mars atakuwa anazidi kufungua Champagne kufuatia mafanikio ambayo amekuwa akiyapata kila kukicha pamoja na mkwanja ambao ameingiza kwenye ziara yake ya dunia ya muziki iliyoanza March 28 huko Antwerp, Ubelgiji na kumalizika Nov. 11 huko Inglewood, Calif.

Msanii huyo ametajwa kuingiza kiasi cha dola milioni 240 kupitia ziara yake ya muziki ya ’24K Magic World Tour’ iliyoanza March 28, 2017 ambapo ni sawa na tiketi milioni 2.3 zilizouzwa.

Mars ametajwa kuingiza kiasi cha dola milioni 28 kupitia tiketi zilizouzwa kwenye nchi za Latin America na Australia.

kwa mujibu wa box office, jumla ya kiasi cha dola milioni 15.7 kiliinia kwenye show hizo ambapo ni sawa na wastani wa watu 178,989 waliohudhuria.

Kupitia ziara hiyo Bruno Mars aliwahi kuuza tiketi milioni 1 ndani ya siku moja, kwa mujibu wa Live Nation.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents