Michezo
Wayne Rooney aivunja rekodi ya Sir Bobby Charlton
Mchezaji wa Uingereza, Wayne Rooney, usiku wa September 8 aliivunja rekodi ya Sir Bobby Charlton kwa kufunga goli la 50.
Wayne Rooney alifunga goli la 50 kwa mkwaju wa penati wakati wa mchezo dhidi ya Switzerland wa kuwania kufuzu kucheza EURO 2016. Mechi hiyo ilimalizika kwa Uingereza kuibuka na ushindi wa jumla wa goli 2-0.
Baada ya mechi hiyo kumalizika Rooney aliingia katika chumba cha kubadilishia nguo na kuanza kupigiwa makofi na wachezaji wenzake. Kocha wake alimkabidhi jezi namba 50 ambayo ni jumla ya magoli aliyofunga katika timu ya taifa ya Uingereza.