Michezo
Wayne Rooney ateuliwa kuwa nahodha mpya Manchester United
Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal amemtangaza Wayne Rooney kuwa nahodha mpya wa timu hiyo na Darren Fletcher kuwa msaidizi wake.
Kwenye maelezo yake Louis van Gaal alisema: Kwangu mimi ni muhimu uteuzi wa nahodha ni kitu muhimu. Wayne ameonesha tabia nzuri katika kila anachokifanya. Nimevutiwa na weledi wake na tabia yake katika mazoezi na falsafa yangu. Ni mfano mzuri kwa wachezaji wachanga katika timu na naamini ataweka moyo wake katika kazi ya unahodha.