Michezo
Wayne Rooney yupo kwenye mazungumzo ya kusaini mkataba mpya na Man United
Mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney ameanza mazungumzo ya kusainimMkataba mpya na Manchester United. Mkataba huo utakuwa wa miaka mitano na atalipwa £300,000 kwa wiki.
Mtandao wa Telegraph umeandika, mkataba huo utamweka Rooney, Old Trafford hadi 2018 na kuashiria kuwa amevitosa vilabu vya Chelsea, Real Madrid na Arsenal vilivyokuwa vikimuwinda.
Inadaiwa kuwa Rooney, ambaye mara mbili ilidaiwa anataka kuihama Man United na Chelsea kutoa ofa mbili mwanzoni mwa msimu ili kumnunua, aliwaamrisha mawakala wake kuanza kuzungumza na uongozi wa timu hiyo mwanzoni mwa mwezi huu kuhusu mkataba mpya. Katika mkataba wa sasa Rooney analipwa £250,000 kwa wiki.