Habari
Waziri Lugola aagiza kushushwa vyeo Mkuu wa usalama barabarani na Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto (+video)
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameagiza Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, kumshusha cheo hadi kubaki na nyota tatu, mkuu wa usalama barabarani, Mbeya, Leopold Fungu. Pia ameagiza Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto mkoa wa Kagera, George Mrutu ashushwe cheo mara moja.
Lugola ameyasema hayo katika Mkutano wake na waandishi wa habari, leo July 6, 2018.