Habari

Waziri Lugola amuonya mwanaharakati Cyprian Musiba ‘Asivuke mipaka, Asione yuko juu ya sheria’ – Video

Waziri Lugola amuonya mwanaharakati Cyprian Musiba 'Asivuke mipaka, Asione yuko juu ya sheria' - Video

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola amepiga biti n akumuonya mwanaharakati Cyprian Musiba juu ya harakati zake anazozifanya maana watu wasione anatumwa na Serikali:

Namuonya mwanaharakati huru Cyprian Musiba ambaye mara kadhaa amekuwa akijaribu kuonyesha Watanzania kwamba pengine Serikali imemtuma pengine Rais imemtuma nataka kuwaamisha watanzania kwamba Serikali haiwatumi wanaharakati, Serikali haimtumi Cyprian Musiba pale ambapo Jeshi la Polisi tutabaini kwamba Cyprian Musiba anaendelea kujiwasilisha katika mazingira yanayoashiria kuwajengea hofu Watanzania kwamba maneno anayoyasema au shughuli zake anazozifanya anatumwa na Serikali tutachukua hatua kali bila kuonenana huruma. Natumia fursa hii kumuonya Cyprian Musiba asivuke mipaka ya shughuli zake aendelea na uanaharakati wake”

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents