Habari
Waziri Lukuvi awasimamisha kazi watumishi 183, majina 20 kufikishwa kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewasimamisha kazi watumishi 183 wa Wizara yake kupisha uchunguzi wa tuhuma za kuingilia mfumo wa kukadiria na kukusanya kodi ya pango la ardhi kinyume na taratibu na kusababisha upotevu wa mapato ya Serikali.
Waziri Lukuvi amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwasilisha orodha hii kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU leo ili uchunguzi uanze mara moja.
Chanzo cha habari hii ni Azam Tv.