Habari
Waziri Mhagama avitaka vyombo vya ulinzi kutupia jicho sekta za madini zinazolindwa na kampuni binafsi za ulinzi
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,, Bunge, Kazi, Vijana,Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akifungua semina ya siku mbili kwa vyombo vya ulinzi na Usalama juu ya ushiriki wa vyombo vya ulinzi na Usalama nchini katika usimamizi na udhibiti wa rasilimali Madini Tanzania.
Katika hotuba yake Waziri Mhagama amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kutupia jicho utaratibu wa baadhi ya wawekwezaji katika sekta ya madini kulindwa na kampuni za ulinzi za binafsi.
Semina hii inafanyika jijini Dodoma na kushirikisha makamanda wa Polisi wa Mikoa yote ya Tanzanzania na Makamanda wa Wilaya na vyombo vingine vya ulinzi na Usalama.
Na Jacquline Ngoya