Habari

Waziri mkuu wa Korea Kusini ajiuzulu kufuatia kuzama kwa ferry iliyosababisha vifo vya watu 187

Waziri mkuu wa Korea Kusini Chung Hong-won amejiuzulu kufuatia kuzama kwa Ferry ya Sewol iliyokuwa na jumla ya abiria 476 wengi wao wakiwa ni wanafunzi na walimu, huko pwani ya kusini ya nchi hiyo wiki iliyopita.

korea meli-1

“vilio cha familia za wale ambao bado hawajaonekana vinanikosesha usingizi usiku” alisema Chung Hong-won.
Maafisa wa Korea Kusini wamethibitisha jumla ya watu 187 walipoteza maisha katika ajali hiyo.

Wakati akitoa taarifa ya kujiuzulu alisema kitu sahihi anachotakiwa kufanya sasa ni kuwajibika na kujiuzulu kutokana na kile kilichotokea, na kuomba radhi kwa niaba ya Serikali.

korea
Baadhi ya wakazi wa Korea Kusini wakimtazama Waziri mkuu wakati akijiuzulu

Haya ndio maneno ya Mr Chung aliyoyasema kupitia televisheni:

“The right thing for me to do is to take responsibility and resign as a person who is in charge of the cabinet, on behalf of the government, I apologise for many problems from the prevention of the accident to the early handling of the disaster.”

Aliongeza: “There have been so many varieties of irregularities that have continued in every corner of our society and practices that have gone wrong. I hope these deep-rooted evils get corrected this time and this kind of accident never happens again.”

Rais Park Geun-hye wa Korea Kusini amekubaliana na kujiuzulu wa waziri mkuu wake.

Source: BBC

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents